22 Lakini waovu wataondolewa katika inchi, na watu wabaya watangolewa toka ndani yake.
Tena leo hii, Yawe ataweka mufalme mwingine katika Israeli ambaye ataua watu wa jamaa ya Yeroboamu.
Saulo alikufa kwa sababu ya kutokuwa mwaminifu; hakukuwa mwaminifu maana hakutii neno la Yawe na alikwenda kwa mwaguzi kumwomba shauri,
Mwovu anaponyeshwa siku ya hasara, anaokolewa siku ya kasirani!
Wenye zambi wote waondolewe katika dunia, waovu wote wasikuwe tena! Umusifu Yawe, ee nafsi yangu! Haleluia!
Yawe anawalinda wote wanaomupenda; lakini anawaangamiza waovu wote.
Lakini waovu wataangamia, waadui za Yawe watanyauka kama maua katika jangwa; kweli watatoweka kama moshi.
Waliobarikiwa na Yawe watarizi inchi, lakini waliolaaniwa naye wataongolewa.
maana Yawe anapenda haki, wala hawaachi waaminifu wake. Anawalinda hata milele; lakini wazao wa waovu wataangamizwa.
Wewe unapenda ubaya kuliko uzuri, unapenda uongo kuliko ukweli.
Kwa hiyo Mungu atakuangamiza milele, atakunyanyua na kukuondoa katika nyumba yako; atakuongoa katika inchi ya wenye kuishi.
Wenye haki hawataondolewa katika inchi hata kidogo, lakini waovu hawatakaa katika inchi.
Ukamilifu wa watu wa usawa unawaongoza. Upotovu wa wadanganyifu unawaangamiza.
Yawe atamutenga kutoka kati ya makabila yote ya Israeli apatwe na hasara kufuatana na laana zote za agano zilizoandikwa katika kitabu hiki.
“Mambo ya siri ni ya Yawe, Mungu wetu, lakini yale ambayo ameyafunua ni yetu na wazao wetu milele, kusudi tushike maneno yote ya sheria hii.”
Yawe, Mungu wenu, atafukuza mataifa haya kadiri munavyosonga mbele kidogokidogo. Hamutaweza kuyaangamiza yote kwa mara moja, kwa sababu mukifanya hivyo hesabu ya nyama wa pori itazidi na kuwa kitisho kwenu.