Yesu akawaambia: “Mwangaza ungali kati yenu kwa muda kidogo. Mutembee wakati mungali na mwangaza, kusudi giza lisiwafunike, kwa sababu anayetembea katika giza hajui pahali anapokwenda.
Ijapokuwa wanamujua Mungu, hawamutukuzi wala kumushukuru kama vile anavyostahili. Lakini mawazo yao yaligeukia mambo ya ovyo ovyo, na mioyo yao isiyokuwa na ufahamu ilibaki katika giza.
Watu hawa wametoka kati yetu, lakini hawakukuwa wa kundi letu, na kwa sababu hii wametuacha. Kama wangekuwa wa kundi letu, wangekaa pamoja nasi. Lakini wametuacha kusudi ionekane wazi ya kama hawakukuwa wa kundi letu.