Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 19:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Anayeshika amri analinda maisha yake; anayezarau agizo atakufa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 19:16
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kweli mahangaiko yanamwua mupumbafu, na wivu unamwangamiza mujinga.


kwa wote wanaoshika agano lake, wanaokumbuka kutii amri zake.


Anayezarau mashauri anajiletea maangamizi, lakini anayetii amri atapewa zawadi.


Anayekataa kufundishwa anajizarau mwenyewe, lakini anayekubali maonyo anapata ufahamu.


Njia ya watu wa usawa ni kujiepusha na uovu; anayechunga njia yake anachunga maisha yake.


Anayetangatanga mbali na njia ya ufahamu, atajikuta ametua kati ya wafu.


Anayechunga kinywa chake na ulimi wake, anajiepusha na matatizo.


Njia ya waovu imejaa miiba na mitego; anayetaka kulinda maisha yake ataiepuka.


Pasipo maono ya kinabii, watu wanashindwa kujizuiza. Heri mutu yule anayeshika sheria.


Mwana wangu, usisahau mafundisho yangu, lakini kwa moyo wako ushike amri zangu.


Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.


Anayetii amri hatapata hasara, na mwenye hekima atajua kwamba kuna wakati wa hukumu.


Lakini niliwapa amri kwamba waitii sauti yangu kusudi nikuwe Mungu wao, nao wakuwe watu wangu. Niliwaamuru vilevile waishi kama nilivyowaagiza, kusudi wapate uheri.


Maana aliisikia sauti ya baragumu, akazarau onyo; basi lawama itakuwa juu yake mwenyewe. Lakini kama angejali hilo onyo, angeyaokoa maisha yake.


Ni faida gani kwa mutu kupata utajiri wote wa dunia, lakini anapoteza uzima wake? Hakuna kitu mutu anachoweza kutoa kwa kukomboa uzima wake.


Basi Yesu akamwambia: “Umejibu vizuri. Fanya sawa vile unavyosema, nawe utaishi milele.”


Lakini Yesu akajibu: “Heri zaidi wale wanaosikia neno la Mungu na kulitii!”


“Kama munanipenda, mutashika amri zangu.


Kutahiriwa au kutotahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni kutii amri za Mungu.


Nasi tunapokea jambo lolote tunaloomba kwake, kwa sababu tunatii amri zake na kutenda mambo yanayomupendeza.


Kwa maana kumupenda Mungu ni kutii amri zake. Na amri zake si ngumu,


Heri wale wanaosafisha kanzu zao, kwa maana watakuwa na haki ya kukula matunda ya muti wa uzima na ya kuingia katika muji ule kwa kupitia kwenye milango.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ