Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 18:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Si vizuri kumupendelea mutu mwovu, na kumunyima sheria mutu wa haki.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 18:5
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yeye hawapendelei wakubwa, wala kuwajali watajiri kuliko wamasikini, maana wote hao ni kazi ya mikono yake.


“Mpaka wakati gani mutaendelea kuhukumu bila haki na kuwapendelea watu waovu?


Usifuate watu wengi kwa kutenda ubaya. Wala wakati wa kukata maneno, usishuhudie kufuatana na watu wengi kwa kupotosha haki.


Usikuwe na upendeleo katika mashitaki ya masikini.


Usipotoshe haki masikini anayostahili katika mashitaki yake.


Kumuhesabu mwovu kuwa na haki na kumwazibu asiyekuwa na kosa, yote mawili ni chukizo kwa Yawe.


Si vizuri kumwazibu mutu asiyekuwa na kosa; ni kosa kuwapiga fimbo wenye heshima.


Hii ni misemo mingine ya wenye hekima. Kupendelea watu katika hukumu si vizuri.


Si vizuri kumubagua mutu. Watu wanafanya mabaya hata kwa ajili ya mukate.


Wakikunywa watasahau maagizo ya sheria, na kuwanyima haki wenye taabu.


Kwa ajili ya kituliro kidogo wanawaachilia wenye kosa na kuwanyima wasiokuwa na kosa haki yao.


Sheria ya Mungu imewekwa pembeni, haki iko mbali; ukweli unakanyagwa katika tribinali, usawa hauwezi kuingia humo.


Unapotoa hukumu uamue kwa haki, usimupendelee masikini wala kumwogopa mwenye cheo. Lakini hukumu mwenzako kwa haki.


Musikie jambo hili, enyi waongozi wa wazao wa Yakobo, musikilize, enyi watawala wa Waisraeli: Ninyi munachukia sheria ya Mungu na kupotosha mambo ya usawa.


Wote ni wafundi wa kutenda maovu; waongozi na waamuzi wanaomba kituliro. Wakubwa wanaonyesha wazi nia zao mbaya, nao wanashirikiana pamoja kwa kuzitimiza.


Halafu wakatuma kwake wamoja kati ya wanafunzi wao pamoja na watu wengine wamoja waliojiunga na Herode kumwuliza maneno haya: “Mwalimu, tunajua kuwa wewe ni mutu wa kweli na kwamba unafundisha kwa kweli njia Mungu anayoamuru. Vilevile haushuguliki na mafikiri ya mutu yeyote kwa sababu hauangalii cheo cha mutu.


Musipotoshe haki, musikuwe na upendeleo, wala musikubali kupokea kituliro, kwa kuwa kituliro kinapofusha macho ya watu wenye hekima na kupotosha maneno ya mutu mwenye haki.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ