Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 18:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Masikini anaomba kwa unyenyekevu, lakini tajiri anajibu kwa ukali.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 18:23
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu munaonyesha heshima kwa yule anayevaa vizuri na kumwambia: “Ikaa hapa kwenye nafasi nzuri.” Lakini munamwambia yule masikini: “We! Simama pale, au uikae hapa chini kwenye nafasi ya kuwekea miguu yangu.”


Lakini ninyi munawazarau wamasikini! Watajiri si ndio wale wanaowagandamiza ninyi na kuwashitaki kwenye tribinali?


“Heri wale wanaokuwa wamasikini wa roho, maana Ufalme wa mbinguni ni kwao!


Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Sasa ufikiri juu ya jambo hili na uamue la kufanya. Jambo hili linaweza kuleta hasara kwa bwana wetu na jamaa yake yote. Yeye ni mutu mubaya na hakuna anayeweza kusema naye.”


Kisha Nabali akawajibu watumishi wa Daudi: “Daudi ni nani? Mwana wa Yese ni nani? Siku hizi kuna watumishi wengi wanaowakimbia wabwana zao.


Yeyote atakayebakia katika jamaa yako atamwendea kuhani yule na kumwomba kikoroti cha feza au mukate, na kumwambia: Ninakuomba uniweke kwenye nafasi moja ya kuhani kusudi niweze kupata tu kipande cha mukate.”


Aliniomba nimuruhusu awafuate nyuma wavunaji naye akiokota masalio kati ya miganda. Basi alikuja na amefanya kazi tangu asubui na ni sasa tu amekwenda kupumzika katika kibanda.”


Lakini mufalme wa Misri akawauliza: “Ni nani yule Yawe, hata nimusikilize na kuwaacha Waisraeli waondoke? Mimi simujui yule Yawe, wala sitawaruhusu Waisraeli waondoke.”


“Mukubwa wa inchi ile alisema nasi kwa ukali, na kutuona kwamba sisi ni wapelelezi katika inchi yake.


Yosefu alipoona kaka zake akawatambua, lakini akajifanya sawa vile hawafahamu, akasema nao kwa ukali. Akawauliza: “Mumetoka wapi ninyi?” Wakamujibu: “Tumetoka katika inchi ya Kanana, tumekuja kununua chakula.”


Mufalme akawajibu watu hao kwa ukali, akazarau shauri alilopewa na wazee,


Naye mufalme Rehoboamu akawajibu kwa ukali, akazarau shauri la wazee,


Masikini anachukiwa na wandugu zake; warafiki zake ndio zaidi: wanamukimbia! Hata awabembeleze namna gani, hatawapata.


Tajiri anamutawala masikini. Mwenye kukopesha ni mutumwa wa mwenye kukopeshwa.


Nani aliyenipa kitu, kusudi nipate kumurudishia? Chochote kinachokuwa chini ya mbingu ni changu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ