11 Tajiri anazani kwamba mali ni makimbilio yake; anafikiri hayo ni ukuta murefu unaomulinda.
Mali ya tajiri ndiyo kikingio chake. Umasikini wa masikini unamuletea maangamizi.
Utajiri haufai kitu siku ya kasirani, lakini haki inaokoa kutoka kifo.
Majivuno ya ndani ya moyo yanaleta maangamizi, lakini unyenyekevu unaleta heshima.
Tajiri anajiona mwenyewe kuwa mwenye hekima, lakini masikini mwenye akili atamufichua.
Kulindwa na hekima ni kama kulindwa na feza. Faida ya maarifa ni kwamba hekima inalinda maisha ya mutu anayekuwa nayo.
Yawe anasema hivi: Mwenye hekima asijivunie hekima yake, mwenye nguvu asijivunie nguvu yake; wala tajiri asijivunie utajiri wake.
Hata waadui zetu wenyewe wanajua wazi, mulinzi wao hana nguvu kama mulinzi wetu.