Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 18:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Jina la Yawe ni munara imara; mwenye haki anaukimbilia na kuwa salama.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 18:10
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati Abramu alipokuwa na umri wa miaka makumi tisa na tisa, Yawe akamutokea, akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Uwezo. Uendelee mbele yangu na kuwa mukamilifu.


sistahili hata kidogo wema wote na uaminifu wote ulionitendea mimi mutumishi wako. Nilipovuka muto Yordani, sikukuwa na kitu isipokuwa fimbo; lakini sasa nina makundi haya mawili.


Alisema: Yawe ni: kikingio changu, kimbilio langu, mukombozi wangu,


Mungu wangu, yule ambaye ninamukimbilia, ngao yangu, nguvu ya wokovu wangu, munara wangu, kimbilio langu. Mwokozi wangu, unaniokoa kutoka watesaji wakali!


Mungu anamujalia mufalme wake ushindi mukubwa; anamutendea mema muchaguliwa wake, ndiye Daudi na wazao wake milele.


rafiki yangu wa kweli, kimbilio langu, upango wangu, mukombozi wangu, ngao yangu, yule anayenilinda, yule anayeshinda mataifa na kuyaweka chini yangu.


Yawe akujibu unapokuwa katika taabu; jina la Mungu wa Yakobo likulinde.


Zaburi ya Daudi. Yawe ni mwangaza wangu na wokovu wangu, ni nani nitakayemwogopa? Yawe ni mulinzi wa maisha yangu, sitamwogopa mutu yeyote.


Mungu anasema: “Nitamwokoa yule anayenipenda; nitamulinda anayejua jina langu!


utaweza kumwambia Yawe: “Wewe ni kimbilio langu ninamojificha, Mungu wangu ninayemutumainia!”


Nilimutokea Abrahamu, Isaka, na Yakobo nikijulikana kama Mungu Mwenye Nguvu, ingawa sikuwajulisha jina langu, Yawe.


Anayemwogopa Yawe ana tumaini imara, na watoto wake watapata kimbilio salama.


Kuogopa watu ni kujitega mwenyewe, lakini anayemutumainia Yawe yuko salama.


Mutumainie Yawe siku zote kwa maana yeye ni kikingio chetu kwa milele.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Katika siku za utawala wake, inchi ya Yuda itaokolewa na inchi ya Israeli itakuwa katika usalama. Naye ataitwa kwa jina la Yawe Ni Haki Yetu.


Bwana, Yawe ndiye nguvu yangu, anaimarisha miguu yangu kama ya paa, ananiwezesha kupita juu katika milima. Kwa mwimbishaji: pamoja na ala za muziki wa nyuzi.


“Angalia bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume, naye ataitwa Emanueli,” (maana yake “Mungu yuko pamoja nasi”).


Bwana Mungu Mwenye Uwezo anasema: “Mimi ni Alfa na Omega.” Ni yeye anayekuwa, aliyekuwa na anayekuja.


Lakini Daudi akamwambia Goliati: “Wewe unanifikia kwa upanga na mikuki. Lakini mimi ninakufikia kwa jina la Yawe wa majeshi, Mungu wa waaskari wa Israeli, ambaye wewe umemutukana.


Sasa, Daudi alikuwa katika matatizo makubwa kwa sababu watu wake walikuwa na uchungu katika roho zao kwa kupoteza watoto wao. Kwa hiyo wakakuwa wakitaka kumupiga mawe. Lakini Daudi alijipa moyo kwa kumutegemea Yawe, Mungu wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ