Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 17:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kwa anayetoa kituliro ni kama hirizi; kila kitu anachofanya yeye anafanikiwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 17:8
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yakobo akalala pale usiku ule. Kisha akatenga sehemu ya mali yake, ikuwe zawadi kwa ndugu yake Esau:


Zaidi ya yote, mutamwambia: ‘Mutumishi wako Yakobo yuko nyuma, anafuata.’ ” Yakobo alifanya hivyo akifikiri: “Pengine nitamutuliza kwa zawadi hizi ninazomutangulizia na kisha nitaweza kuonana naye macho kwa macho; labda atanipokea.”


Hapo Israeli, baba yao, akawaambia: “Basi! Kwa vile ni lazima ikuwe hivyo basi, mufanye hivi: mutwae katika mifuko yenu sehemu ya mazao bora ya inchi yetu, mumupelekee zawadi yule mukubwa. Mumupelekee mafuta kidogo ya mukwaju, asali kidogo, ubani, marasi, kungu na lozi.


Ee Yawe, ulipovikaripia, pumzi ya pua yako ilifunua vilindi vya bahari na misingi ya dunia ikaonekana.


nalo linatoka kama vile bwana-arusi kutoka chumba chake, linakimbia kwa furaha katika njia yake kama shujaa.


Kwa maana wewe utapiga mishale mbele yao, utawakimbiza mbio.


Sauti ya Yawe ni yenye nguvu, sauti ya Yawe ni yenye mamlaka.


Usipokee kituliro, maana kituliro kinapofusha wakubwa na kupotosha mambo ya wenye haki.


Mutu mubaya anapokea kituliro kwa siri kusudi apate kupotosha haki.


Zawadi inamufungulia mutu milango; inaweza kumufikisha mutu mbele ya mukubwa.


Hasira inatulizwa kwa zawadi ya siri; kituliro kinachotolewa kwa uficho kinatuliza kasirani.


Mwenye hekima akimutesa mutu, yeye anafanya kama mupumbafu. Kupokea kituliro kunapotosha akili.


Wakubwa wako ni waasi; wanashirikiana na wizi. Kila mumoja anapenda kituliro, na kukimbilia zawadi. Hawamupatii yatima haki yake, haki za wajane si kitu kwao.


Maana mimi ninajua wingi wa makosa yenu na ukubwa wa zambi zenu; ninyi munawatesa watu wema, munapokea kituliro na kuzuia wakosefu wasipate haki katika tribinali.


Wote ni wafundi wa kutenda maovu; waongozi na waamuzi wanaomba kituliro. Wakubwa wanaonyesha wazi nia zao mbaya, nao wanashirikiana pamoja kwa kuzitimiza.


Musipotoshe haki, musikuwe na upendeleo, wala musikubali kupokea kituliro, kwa kuwa kituliro kinapofusha macho ya watu wenye hekima na kupotosha maneno ya mutu mwenye haki.


Kisha, Daudi akapokea vitu vyote ambavyo Abigaili alikuwa amemuletea, akamwambia Abigaili: “Rudi kwako na amani. Mimi nimeyasikia uliyosema, na ombi lako nimelipokea.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ