Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 17:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Zahabu na feza vinapimwa kwa moto, lakini Yawe ndiye anayepima mioyo ya watu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 17:3
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninajua, Mungu wangu, kwamba wewe unapima moyo, nawe unapendezwa na uaminifu. Nami, katika uaminifu wa moyo wangu nimetoa vitu hivi vyote kwa mapenzi yangu, na sasa ninaona watu wako wanaokuwa hapa, wakikutolea kwa mapenzi yao na furaha.


Lakini yeye anajua njia ninayofuata; atakapomaliza kunipima nitatoka mule safi kama zahabu.


Hakika kuna nafasi ya kuchimba feza, na pahali ambako zahabu inasafishwa.


Unichunguze, ee Mungu, unijue moyo wangu, unipime, uyajue mawazo yangu.


Unijaribu, ee Yawe, na kunipima; uchunguze moyo wangu na akili yangu.


Umetupima, ee Mungu, umetujaribu kama madini kwa moto.


Ikiwa Yawe anajua kuzimu na shimo la kuangamia, mawazo ya mwanadamu yataweza namna gani kujificha mbele yake?


Matendo yote ya mutu yanaonekana kwake kuwa sawa lakini Yawe anapima nia ya mutu.


Mutumwa mwenye hekima atatwaa nafasi ya mwana mupumbafu. Atapata sehemu ya urizi wa jamaa hiyo.


Matendo yote ya mutu ni sawa katika macho yake, lakini Yawe anapima mioyo.


Zahabu na feza vinapimwa kwa moto, na mutu anapimwa kutokana na sifa zake.


Mimi nimekusafisha lakini si kama feza katika furu. Nimewapima katika furu ya taabu.


Mimi Yawe ninapima akili na kuchunguza moyo wa mutu. Na hivyo ninamutendea kila mumoja, kulingana na mwenendo wake, kadiri ya matendo yake.


Wewe mwanadamu! Waisraeli wamekuwa kwangu kama takataka. Wao ni kama takataka inayobaki wakati madini ya shaba, bati, chuma au risasi yanaposafishwa.


Wamoja kati ya wenye hekima watauawa, kusudi wapate kuondolewa uchafu, kutakaswa na kusafishwa, mpaka wakati wa mwisho, ambao sasa bado haujatimia.


Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.


Tena ni yeye aliyewakulisha mana katika jangwa, chakula ambacho babu zenu hawajapata kukijua. Alifanya hayo yote kusudi awanyenyekeze na kuwajaribu kwa kuwapima apate kuwajalia mema kwa mwisho.


Mukumbuke jinsi Yawe, Mungu wenu, alivyowaongoza katika safari ndefu kupitia katika jangwa kwa muda wa miaka hiyo makumi ine, kusudi awanyenyekeze na kuwajaribu kusudi ajue yanayokuwa ndani ya mioyo yenu, na kama mungeshika amri zake au hapana.


Majaribu hayo ni kwa ajili ya kupima imani yenu. Zahabu ni kitu kinachoharibika, lakini ingawa vile inapimwa kwa njia ya kuchomwa ndani ya moto. Hivi vilevile imani yenu inayokuwa ya bei kali kuliko zahabu, inapaswa kupimwa kusudi ijulikane kuwa ya kweli. Na kwa sababu hii mutapata sifa, utukufu na heshima wakati Yesu Kristo atakapotokea.


Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ