22 Moyo wenye furaha ni dawa, lakini moyo wenye huzuni unakondesha mwili.
Nimekwisha kama maji yaliyomwangika; mifupa yangu yote imeteguka; moyo wangu ni kama inta, unayeyuka ndani yangu.
Wasiwasi ndani ya moyo inamukosesha mutu raha, lakini neno zuri linamuchangamusha.
Moyo wa furaha unaangarisha uso, lakini uchungu unavunja moyo.
Maneno mazuri ni kama asali. Ni matamu kwa nafsi na yenye kuupatia mwili afya.
Roho ya mutu inaweza kuvumilia ugonjwa, lakini ukiwa umevunjika moyo, utavumilia namna gani?
Nikasema juu ya kicheko: “Ni wazimu”, na raha: “Iko na faida gani?”
Basi sasa ni afazali kumusamehe na kumufariji, na kuepuka asikate kitumaini kwa sababu ya huzuni kubwa.
Basi, huzuni inayosababishwa na Mungu inamuwezesha mutu kugeuka toka katika zambi. Na kugeuka kule, kunamuletea kuokoka. Kule kuokoka hakuleti majuto. Lakini huzuni inayosababishwa na mwanadamu inaleta kifo.