20 Mwenye moyo mupotovu hafanikiwi, na musema uongo anapatwa na hasara.
Wewe ni mwema kwa wema, mukamilifu kwa wakamilifu,
Anayekonyeza macho kwa nia mbaya analeta taabu, lakini anayeonya waziwazi analeta amani.
Wenye hekima wanalinda maarifa, lakini kusemasema kwa mupumbafu kunaleta maangamizi haraka.
Kinywa cha mwenye haki kinatoa mambo ya hekima, lakini ulimi wa mutu mubaya utakatwa mbali.
maana siku mbaya zitamufikia mwovu; taa ya uzima wake itazimika.
Maana waovu ni chukizo kwa Yawe, yeye anawafanya watu wa usawa kuwa warafiki zake.
Kumwogopa Yawe ni kuchukia uovu. Ninachukia kiburi, majivuno maisha mabaya, na luga mbaya.
Maneno ya mwenye hekima yanamupa upendeleo; lakini maneno ya mupumbafu yanamwangamiza.