Jamaa yako nitaifanya kama jamaa ya Yeroboamu mwana wa Nebati, na kama jamaa ya Basha mwana wa Ahiya, kwa sababu umeiwasha hasira yangu na kuwasukuma watu wa Israeli watende zambi.’
Musirudishiane mabaya kwa mabaya au matusi kwa matusi, lakini muombeane baraka, kwa sababu Mungu aliahidi kuwabariki ninyi wakati alipowaita kumufuata.
Yonatani alimusifu Daudi mbele ya baba yake, akamwambia: “Usitende zambi juu ya mutumishi wako Daudi maana yeye hajatenda zambi yoyote juu yako. Matendo yake yote siku zote yamekuwa mazuri kwako.
Daudi alikuwa akifikiri: “Mimi nimekuwa nikilinda mali yote ya Nabali katika jangwa bila faida yoyote na hakuna kitu chake chochote kilichopotea, naye amenilipa mabaya kwa mazuri niliyomutendea.