Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 17:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Nia ya mutu mwovu ni kuasi tu; mujumbe mubaya atatumwa juu yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 17:11
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati Abusaloma alipokuwa akitoa sadaka, alituma ujumbe katika muji wa Gilo kwa kumwita Ahitofeli wa muji wa Gilo, aliyekuwa mushauri wa mufalme Daudi. Uasi wa Abusaloma ukazidi kupata nguvu na watu waliojiunga naye wakazidi kuongezeka.


Kisha, vijana kumi waliomubebea Yoabu silaha, wakakuja kumuzunguka Abusaloma, wakamupiga na kumwua.


Kisha, Ahimasi mwana wa Zadoki, akasema: “Uniruhusu nikimbie kumupelekea mufalme habari hizi kwamba Yawe amemukomboa toka katika nguvu za waadui zake.”


Sasa ilitokea kwamba kule Gilgali kulikuwa mutu mumoja wa ovyoovyo anayeitwa Seba mwana wa Bikiri, wa kabila la Benjamina. Basi Seba alipiga baragumu, na kusema: “Hatuna ushirika wowote na Daudi; hatuna sehemu yetu katika huyo mwana wa Yese. Enyi watu wa Israeli, kila mumoja ajiendee katika hema yake!”


Kisha, huyo mwanamuke akaenda kwa watu wote katika muji kwa hekima yake. Wakamukata Seba mwana wa Bikiri kichwa, wakakitupa inje kwa Yoabu. Kwa hiyo, Yoabu akapiga baragumu na kuwatawanya watu wake kutoka muji ule wa Abeli. Kila mutu akaenda kwake. Yoabu akarudi kwa mufalme Daudi, kule Yerusalema.


Solomono akasema: “Fanya sawa alivyosema. Umwue na kumuzika. Hivyo, mimi na wazao wengine wote wa Daudi hatutabeba lazima ya vitendo vya Yoabu vya kuwaua watu wasiokuwa na kosa.


Hapo, mufalme akamwamuru Benaya mwana wa Yehoyada, naye akatoka, akamupiga na kumwua Simei. Basi, ufalme ukaimarika chini ya Solomono.


Onyo kwa mwenye akili lina maana, kuliko mapigo mia moja kwa mupumbafu.


Afazali kukutana na dubu dike aliyenyanganywa watoto wake, kuliko kukutana na mupumbafu katika upumbafu wake.


Mwana wangu, uwaheshimu Yawe na mufalme, wala usishirikiane na waasi,


Nao wakamujibu: “Atawaua hao watu wabaya pasipo huruma, naye atapatana na walimaji wengine kwa kutunza shamba lake na kumupatia sehemu yake ya matunda kwa wakati wa mavuno.”


Halafu mufalme akakasirika. Akawatuma waaskari wake kuwaua wale wauaji na kuteketeza muji wao kwa moto.


Na sasa kwa ngambo ya wale waadui zangu walionikataa mimi kuwa mufalme wao, muwalete hapa na kuwaua mbele yangu.’ ”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ