1 Afazali kula mukate wenye kukauka kwa amani kuliko karamu katika nyumba ya ugomvi.
Afazali mali kidogo ya mutu wa haki kuliko utajiri mwingi wa watu waovu.
Afazali kuwa na kidogo na kumwogopa Yawe, kuliko kuwa na mali nyingi pamoja na taabu.
Afazali kula mboga za majani kwa upendo, kuliko karamu ya nyama nono pamoja na chuki.
Afazali mali kidogo kwa njia ya haki, kuliko mapato mengi kwa njia isiyofuatana na sheria ya Mungu.
Mutumwa mwenye hekima atatwaa nafasi ya mwana mupumbafu. Atapata sehemu ya urizi wa jamaa hiyo.
Afazali kuishi katika jangwa kuliko kukaa na mwanamuke mugomvi na muchokozi.
Afazali kuishi pembeni juu ya paa, kuliko kuishi ndani ya nyumba pamoja na mwanamuke mugomvi.
“Ilinipasa kutoa sadaka zangu; leo hii nimekamilisha naziri yangu.