Basi, Esau akamuchukia Yakobo kwa sababu ya baraka aliyokuwa amepewa na baba yake. Esau akawaza: “Siku za kilio cha baba zitakapokwisha, ndipo nitakapomwua ndugu yangu Yakobo.”
Vilevile wakawapa wasimamizi wa mufalme na watawala wa mukoa wa majimbo ya upande wa magaribi wa muto Furati maagizo waliyopewa na mufalme, nao wakatoa musaada kwa watu na kwa ajili ya nyumba ya Mungu.
Basi, ee Yawe, acha laana hizo zinipate kama sikukutumikia vizuri na kama sikukusihi kwa ajili ya waadui zangu wakati walipokuwa katika taabu na shida!
Kweli nina vitu vyote vya lazima na zaidi kupita. Sasa kwa kuwa Epafrodito ameniletea zawadi zenu zote, ninatosheka. Zawadi hizi ni kama sadaka ya ubani yenye harufu nzuri, na kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto inayokubaliwa na Mungu na kumupendeza.
Hivi, mutaweza kuishi sawa Bwana anavyotaka na kumupendeza katika mambo yote. Kwa njia hiyo mutafikia kufanya matendo mema ya kila namna na kuzidi kumujua Mungu.
awakamilishe katika kila tendo jema kusudi mupate kutimiza mapenzi yake; yeye atimize ndani yetu yale yanayomupendeza, kwa njia ya Yesu Kristo. Yesu atukuzwe milele na milele. Amina.