Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 16:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Anayefikiri sana juu ya neno atafanikiwa. Heri mutu yule anayemutumainia Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 16:20
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Waliweka tumaini lao kwa Mungu na wakamwomba awasaidie, naye akaitikia ombi lao na kuwatia katika mikono yao Wahagari pamoja na warafiki zao.


Wimbo wa safari za kidini. Wanaomutegemea Yawe, wako kama mulima Sayuni, ambao hautikisiki lakini unabaki imara siku zote.


Heri mutu anayesaidiwa na Mungu wa Yakobo, mutu anayemutumainia Yawe, Mungu wake,


Watu waovu watapata mateso mengi, lakini wanaomutumainia Yawe wanazungukwa na wema wake.


Malaika wa Yawe anawalinda wote wanaomwabudu, na kuwaokoa kutoka katika hatari.


Anayezarau mashauri anajiletea maangamizi, lakini anayetii amri atapewa zawadi.


Kuwa na akili kunaleta ukubali, lakini njia ya waovu ni ya taabu.


Mutumwa mwenye hekima atatwaa nafasi ya mwana mupumbafu. Atapata sehemu ya urizi wa jamaa hiyo.


Anayejipatia hekima anapenda nafsi yake; anayeshika ufahamu atastawi.


Anayenipata mimi amepata uzima, na upendeleo kutoka kwa Yawe.


Hata hivyo, Yawe anangoja kuwasamehe, atasimama na kuwaonea huruma. Yawe ni Mungu wa haki. Heri wote wale wanaomutumainia.


Basi, mufalme Nebukadneza akasema: Asifiwe Mungu wa Sadiraki, Mesaki na Abedenego kwa sababu alimutuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake ambao wanamutegemea. Wao walikataa kutii amri yangu ya kifalme, wakaitoa miili yao kama sadaka pahali pa kuabudu mungu mwingine, lakini Mungu wao peke yake.


Mungu wangu alileta malaika wake kwa kufunga vinywa vya simba hawa, nao hawakunizuru. Alifanya hivyo kwa sababu alijua mimi sina kosa lolote mbele yake na wala sijafanya jambo lolote baya mbele yako.


“Muangalie! Ninawatuma kama kondoo katikati ya imbwa wa pori. Basi mukuwe waangalifu kama nyoka na wakamilifu kama njiwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ