Halafu wakubwa wale walipomwona Yosafati, wakasema: “Huyu ndiye mufalme wa Israeli.” Kwa hiyo, wakamwelekea kwa kumushambulia; lakini Yosafati akapiga kelele, na Yawe akamwokoa. Mungu akawaondoa wale waliokuwa karibu kumushambulia.
Ee Bwana, usikilize maombi yangu mimi mutumishi wako na ya watumishi wako wanaofurahia kukutii wewe. Ninakuomba unifanikishe leo, mimi mutumishi wako, na kunijalia kuhurumiwa na mufalme.” Mimi nilikuwa na madaraka ya kumupa mufalme kinywaji.