Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 15:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 15:8
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati Abusaloma alipokuwa akitoa sadaka, alituma ujumbe katika muji wa Gilo kwa kumwita Ahitofeli wa muji wa Gilo, aliyekuwa mushauri wa mufalme Daudi. Uasi wa Abusaloma ukazidi kupata nguvu na watu waliojiunga naye wakazidi kuongezeka.


Ninajua, Mungu wangu, kwamba wewe unapima moyo, nawe unapendezwa na uaminifu. Nami, katika uaminifu wa moyo wangu nimetoa vitu hivi vyote kwa mapenzi yangu, na sasa ninaona watu wako wanaokuwa hapa, wakikutolea kwa mapenzi yao na furaha.


Upokee maombi yangu kama ubani; ninapoinua mikono yangu kwako, unikubali kama sadaka ya magaribi.


Maombi ya Daudi. Ee Yawe, usikie ombi langu la haki, usikilize kilio changu, uyategee sikio maombi yangu yasiyokuwa ya udanganyifu.


Kitu mutu mwovu anachoogopa ndicho kitakachomupata, lakini kitu mwenye haki anachotamani ndicho atakachopewa.


Yawe anajiweka mbali na watu waovu, lakini yuko karibu na wenye haki kwa kuwasikiliza.


Mudomo wa mwenye hekima unaeneza maarifa, lakini sivyo kwa mioyo ya wapumbafu.


Sadaka ya mwovu ni kitu cha kuchukiza sana. Inachukiza zaidi akiitoa kwa nia mbaya.


Kutenda mambo ya haki na kufuata sheria ya Mungu kunamupendeza Yawe kuliko sadaka.


Anayekataa kuisikia sheria, yule, hata maombi yake, ni chukizo kwa Mungu.


Fikiri mbele ya kusema, wala usikuwe mwepesi kwa kusema neno lolote mbele ya Mungu, kwa maana Mungu yuko mbinguni na wewe uko katika dunia. Kwa hiyo usiseme maneno mengi.


Ee njiwa yangu, uliyejificha katika matundu kwenye mulima, uniache kuona uso wako na kusikia sauti yako, maana sauti yako ni nzuri na uso wako unapendeza.


Mimi Yawe ninapenda watu wafuate sheria yangu; ninachukia unyanganyi na uovu. Nitawatunza watu wangu kwa uaminifu, nitafanya nao agano la milele.


Lakini watu hawa wanafanya wanavyotaka: wananitolea sadaka ya ngombe na tena wanaua watu kwa kutambikia. Wananitolea sadaka ya mwana-kondoo na vilevile wanaua imbwa. Wananitolea sadaka ya unga na vilevile wanatolea damu ya nguruwe. Wanachoma ubani mbele yangu na kwenda kuabudu miungu ya uongo. Hao wamechagua kufuata njia zao wenyewe.


Kwa nini kuniletea ubani kutoka Seba, na udi wa harufu nzuri kutoka inchi ya mbali? Sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto hazikubaliki, wala sadaka zenu zingine hazinipendezi.


Ulipoanza kuomba, Mungu alitoa jibu, nami nimekuja kukuelezea jibu hilo kwa sababu unapendwa sana. Kwa hiyo, usikilize kwa uangalifu jibu hilo na kuelewa maono hayo.


Kama nyama yoyote ya sadaka ya amani inakuliwa kwa siku ya tatu, mutu aliyeitoa hatakubaliwa, wala hiyo sadaka haitapokelewa kwa faida yake. Nyama hiyo ni chukizo na mutu atakayeikula atabeba lazima ya uovu wake.


Nimwendee Yawe na kitu gani, nipate kumwabudu Mungu anayekuwa juu? Nimwendee na sadaka za kuteketezwa kwa moto, nimutolee mwana-ngombe wa mwaka mumoja?


Yawe atapendezwa nikimutolea maelfu ya kondoo dume, au mito elfu na elfu ya mafuta? Nimutolee muzaliwa wangu wa kwanza kwa ajili ya kosa langu, mutoto wangu wa kwanza kwa ajili ya zambi yangu?


Hagai akajibu na kusema hivi: Hivi ndivyo inavyokuwa kwa watu wa taifa hili mbele yangu –ni ujumbe wa Yawe– na kila kitu wanachofanya; hata vitu wanavyotoa kwenye mazabahu ni vichafu.


Heri kungepatikana mutu mumoja kati yenu ambaye angefunga milango ya hekalu kusudi musiwashe moto usiokubaliwa kwenye mazabahu yangu! Sipendezwi nanyi na sitaikubali sadaka yoyote munayonitolea.


Mungu ni roho, nao wanaomwabudu wanapaswa kumwabudu katika roho na ukweli.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ