Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 15:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Mudomo wa mwenye hekima unaeneza maarifa, lakini sivyo kwa mioyo ya wapumbafu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 15:7
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitarudiliarudilia kwa sauti maamuzi yako yote uliyotoa.


Mutu wa haki anasema maneno ya hekima, kwa ulimi wake anasema kufuatana na sheria ya Mungu.


Moyo wangu umejaa mawazo mazuri: ninamutungia mufalme mashairi yangu, ulimi wangu ni kama kalamu ya mwandishi hodari.


Ulimi wa mwenye hekima unaeneza maarifa, lakini watu wapumbafu wanamwanga maneno ya ujinga.


Katika nyumba ya mwenye haki kuna wingi wa mali, lakini mapato ya waovu yanaleta hasara.


Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


Moyo wa mwenye hekima unamwezesha kusema kwa hekima; unayafanya maneno yake yakuwe ya kuvutia.


Kwa hiyo, utaweza kulinda akili, na kinywa chako kitashika maarifa.


Moyo wa mwenye hekima unamwongoza kutenda mambo yanayokuwa sawa; lakini mutu mupumbafu anapotoshwa na moyo wake.


Midomo yako inadondosha asali, ee muchumba wangu, ulimi wako una asali na maziwa. Harufu nzuri ya nguo zako ni kama miti ya Lebanoni.


Neno ninalowaambia katika giza, muliseme muchana kati. Vilevile neno munalosikia kwa siri, mulitangaze mukisimama juu ya paa ya nyumba.


Ninyi kikundi cha nyoka! Namna gani ninyi munaokuwa wabaya, munaweza kusema maneno mazuri? Kwa maana kinywa kinasema maneno yanayojaa ndani ya moyo.


Kisha akawaambia: “Mwende katika dunia yote na kuhubiri Habari Njema kwa kila mutu.


Musiseme neno lolote baya, lakini kama ni lazima museme tu maneno mazuri na ambayo yanasaidia kuwajenga wengine na yanayoleta neema kwa wale wanaoyasikia.


Wewe umesikia mafundisho niliyotoa mbele ya washuhuda wengi. Nawe sasa uyafundishe kwa watu waaminifu watakaoweza vilevile kuyatoa kwa watu wengine.


Nao ulimi ni kama moto. Ulimi ni kiungo kinachojaa ubaya wa kila namna. Ulimi unapatikana kwenye nafasi yake katikati ya viungo vyetu, nao ndio unaochafua mwili wote. Unateketeza maisha yetu ukichomwa wenyewe na moto unaotoka katika jehenamu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ