6 Katika nyumba ya mwenye haki kuna wingi wa mali, lakini mapato ya waovu yanaleta hasara.
Ndani ya nyumba yake kutakuwa mali nyingi; haki yake utadumu milele.
Afazali mali kidogo ya mutu wa haki kuliko utajiri mwingi wa watu waovu.
Baraka za Yawe ndizo zinazoleta utajiri. Juhudi za mutu haziongezi kitu.
Mutu muzuri anawaachia wazao wake urizi, lakini mali ya mwenye zambi imelundikiwa wenye haki.
Afazali kuwa na kidogo na kumwogopa Yawe, kuliko kuwa na mali nyingi pamoja na taabu.
Mupumbafu anazarau mafundisho ya baba yake, lakini anayekubali maonyo ni mwenye akili.
Mudomo wa mwenye hekima unaeneza maarifa, lakini sivyo kwa mioyo ya wapumbafu.
Afazali mali kidogo kwa njia ya haki, kuliko mapato mengi kwa njia isiyofuatana na sheria ya Mungu.
Katika nyumba ya mwenye hekima kuna hazina za bei kali, lakini mupumbafu anaponda mali yake yote.
Yawe analaani nyumba za waovu, lakini anabariki makao ya wenye haki.
Ninawatajirisha wale wanaonipenda, ninajaza tele hazina za wanaonipenda.
Ni afazali kuwa na kidogo tu, pamoja na amani ndani ya moyo, kuliko kutoa jasho kwa ajili ya kukamata upepo.
Aliona kwamba kupatishwa haya kwa ajili ya Kristo kuna faida kubwa zaidi kuliko kupata utajiri wote wa inchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia kupokea zawadi yake.