22 Mipango inaharibika kwa kukosa shauri, lakini kwa washauri wengi, inasimama.
Basi, kama ukitaka kuyaokoa maisha yako na ya mwana wako Solomono, ninakushauria hivi:
Daudi akashauriana na majemadari wa makundi ya maelfu na makundi ya mamia, pamoja na viongozi wote.
Pasipo uongozi taifa linaanguka; kwenye kuwa washauri wengi kuna usalama.
Upumbafu ni furaha kwa mutu asiyekuwa na akili, lakini mwenye akili anachagua njia inayokuwa sawa.
Kutoa jibu zuri kunafurahisha; neno linalofaa kwa wakati wake ni jema sana!
Mipango mizuri inafanyika kwa kushauriana; ukitaka kuanza vita inafaa kufikiri kwanza.
Maana kwa mipango mizuri unaweza kupigana vita, na kwa washauri wengi ushindi unapatikana.
Kweli, kila kitu kina wakati wake na njia yake, ingawa mwanadamu anapatwa na tatizo kubwa.