Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 15:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Mutu wa hasira mbaya anasababisha ugomvi, lakini asiyekuwa mwepesi wa hasira anautuliza.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 15:18
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wa Yuda wakawaambia watu wa Israeli: “Kwa sababu mufalme ni ndugu yetu wa karibu. Kwa nini munakasirika juu ya jambo hili? Tumekula nini wakati wowote kutoka kwake? Au yeye ametupatia zawadi yoyote?”


Chuki inaleta ugomvi, lakini upendo unafunika makosa yote.


Mutu asiyekuwa mwepesi wa hasira ana akili nyingi, lakini anayekasirika upesi anaongeza upumbafu.


Kujibu kwa upole kunatuliza hasira, lakini neno kali linachochea hasira.


Njia ya muvivu inajaa miiba, lakini njia ya mutu wa usawa ni wazi kama barabara kubwa.


Hasira ya mufalme ni kama mujumbe wa kifo; mutu mwenye hekima ataituliza.


Mutu mupotovu anatawanya ugomvi, na muchonganishi anatenganisha warafiki.


Usifanye urafiki na mutu wa hasira, wala usiandamane na mwenye kukasirika upesi.


Kwa uvumilivu mutawala anaweza kusadikishwa; ulimi laini unavunja mifupa.


Kama vile makaa au kuni vinachochea moto, ndivyo mugomvi anachochea ugomvi.


Muchoyo anachochea magomvi, lakini anayetegemea Yawe atafanikiwa.


Mwenye kasirani anachochea ugomvi, mutu wa hasira anasababisha makosa mengi.


Mutawala akikukasirikia, usiache kazi; makosa makubwa yanaweza kufutwa ukiwa munyenyekevu.


Heri wale wanaoleta amani, maana wataitwa watoto wa Mungu!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ