Naye mufalme wa Israeli akamujibu Yosafati: “Kungali mumoja, Mikaya mwana wa Imula. Yeye tunaweza kumwuliza shauri la Yawe. Lakini ninamuchukia sana kwa sababu yeye hatabiri jambo jema juu yangu hata kidogo, lakini mabaya tu.” Yosafati akamwambia: “Si vizuri kwa mufalme kusema hivyo.”
Maana kutakuja wakati watu watakapokataa kusikiliza mafundisho ya kweli, lakini watafuata tamaa zao wenyewe wakijitafutia walimu wengi kwa kuwafundisha mambo yale wanayotamani kusikia.