Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 15:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Ikiwa Yawe anajua kuzimu na shimo la kuangamia, mawazo ya mwanadamu yataweza namna gani kujificha mbele yake?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 15:11
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

basi usikilize kutokea kule mbinguni, utoe musamaha, vilevile umutendee kila mutu kadiri anavyostahili, (maana ni wewe tu unayejua mawazo ya mioyo ya wanadamu wote),


Kuzimu kuko wazi kabisa mbele ya Mungu. Shimo la kuangamia halina kifuniko chochote.


Nikipanda juu mbinguni, wewe ni kule; nikijilaza chini katika kuzimu, wewe ni kule.


Tungalikuwa tumekusahau wewe Mungu wetu, na kumukimbilia mungu wa uongo,


Wewe, ee Yawe, unayehukumu mataifa, unihukumu kadiri ya haki yangu, kulingana na ukamilifu wangu.


Azabu kali ni kwa wanaoacha mwenendo mwema; yeyote anayechukia kuonywa atakufa.


Zahabu na feza vinapimwa kwa moto, lakini Yawe ndiye anayepima mioyo ya watu.


Kuzimu na shimo la kuangamia havishibi hata kidogo, vilevile macho ya watu hayashibi.


Mimi Yawe ninapima akili na kuchunguza moyo wa mutu. Na hivyo ninamutendea kila mumoja, kulingana na mwenendo wake, kadiri ya matendo yake.


Kisha Yesu akamwuliza mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?” Basi Petro akauzika kwa sababu Yesu alimwuliza mara ya tatu kama anamupenda. Kwa hiyo akamujibu: “Bwana, unajua yote; unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia: “Tunza kondoo wangu.


Kisha wakaomba wakisema: “Bwana, wewe unayejua yanayokuwa ndani ya mioyo ya watu wote, utuonyeshe ni nani uliyemuchagua kati ya hawa wawili


Hakuna kitu kinachoweza kufichwa mbele ya Mungu, lakini vitu vyote vinafunuliwa na viko wazi mbele ya macho yake, yeye tutakayemutolea hesabu ya maneno yetu.


Mimi ni mwenye uzima. Nilikuwa nimekufa, lakini sasa mimi niko muzima kwa milele na milele. Niko na mamlaka juu ya lufu na kuzimu.


Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


Na mufalme wao, ndiye malaika wa lile shimo ndefu la kuzimu, jina lake liliitwa kwa Kiebrania “Abidani” na kwa kigriki “Apolioni” (maana yake “Mwangamizaji”).


Lakini Yawe alimwambia: “Usiangalie sura yake wala urefu wake. Mimi nimemukataa maana siangalii mambo kama vile wanadamu wenye kufa wanavyoangalia. Mwanadamu anaangalia umbo la inje, lakini mimi ninaangalia ndani ya moyo.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ