Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 14:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Amani ndani ya roho inamupa mutu afya, lakini wivu inaozesha mifupa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 14:30
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye akamwambia: “Kwa sababu nilizungumuza na Naboti wa Yezereheli, nikataka aniuzishie shamba lake la mizabibu, au kama akipenda nimupe shamba lingine pahali pa lile. Lakini yeye akaniambia: ‘Sitakupa shamba langu la mizabibu.’ ”


Kweli mahangaiko yanamwua mupumbafu, na wivu unamwangamiza mujinga.


Watu waovu wanaona hayo na kuuzika. Wanasaga meno kwa chuki na kutoweka. Matumaini ya mutu mubaya yanapotea bure.


Moyo wangu ukuwe mukamilifu juu ya masharti yako, kusudi nisifezeheke.


Muke mwema ni taji la utukufu kwa mume wake. Anayemupatisha mume wake haya ni kama kidonda ndani ya mifupa yake.


Moyo wa furaha unaangarisha uso, lakini uchungu unavunja moyo.


Moyo wenye furaha ni dawa, lakini moyo wenye huzuni unakondesha mwili.


Hiyo itakuwa dawa kwa mwili wako, na kitu cha kutuliza mifupa yako.


Linda moyo wako kwa uangalifu wote, maana mule munatokea chemichemi za uzima.


Nikasikia hayo, matumbotumbo yangu yakatetemeka. Midomo yangu inatetemeka kwa hofu, mifupa yangu inateguka, miguu yangu inatetemeka. Ninangojea kwa utulivu siku ile ya hasara, ambayo inawafikia wale wanaotushambulia.


“Wale babu wakamwonea Yosefu wivu hata wakamwuzisha kuwa mutumwa katika inchi ya Misri. Lakini Mungu akamulinda,


Wamejaa kila namna ya uovu, ubaya, tamaa na upotovu. Wamejaa wivu, uuaji, ugomvi, udanganyifu na ukorofi. Wao ni wenye kuchongeana,


Kwa maana Mungu hakutupatia sisi Roho wa kuogopa, lakini Roho anayetupatia nguvu, upendo na kujizuiza.


Musizani kwamba ni kwa bure Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anasikia wivu sana kwa ajili ya yule Roho aliyemuweka akae ndani yetu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ