Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 14:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ndani ya kinywa cha mupumbafu kunatokea maneno ya kiburi, lakini mwenye hekima analindwa na maneno yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 14:3
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Utakingwa salama na mashambulio ya ulimi, wala hautaogopa maangamizi yanapokuja.


Kila mumoja anamudanganya mwenzake; anabembeleza lakini ni kwa moyo wa unafiki.


Usiniache nifezeheke, ee Yawe, maana mimi ninakulilia; lakini uwaache waovu wafezeheke, uwaache wapotelee huko kuzimu.


Atanipelekea musaada toka mbinguni na kuniokoa, atawafezehesha hao wanaonishambulia. Mungu atanionyesha wema na uaminifu wake!


Maneno ya waovu shabaha yake ni kuua, lakini kinywa cha mutu wa usawa kinaokoa.


Anayechunga kinywa chake analinda maisha yake, mwenye midomo mirefu anajiletea maangamizi.


Bila ngombe wa kulima gala za mutu ni tupu. Mavuno mengi yanapatikana kwa nguvu ya ngombe wa kulima.


Maneno ya mupumbafu yanaleta ugomvi; kila neno analosema linasababisha azabu.


Kinywa cha mupumbafu kinamwangamiza mwenyewe; mudomo wake ni mutego wa kumunasa yeye mwenyewe.


Mwenye kiburi na majivuno jina lake ni “Mazarau”; anatenda kwa kujivuna tu.


Anayepanda ubaya atavuna hasara. Uwezo wake wa kutenda mabaya utavunjwa.


Muchoyo anachochea magomvi, lakini anayetegemea Yawe atafanikiwa.


Vilevile nilitaka nielezwe juu ya zile pembe kumi alizokuwa nazo juu ya kichwa chake, na ile pembe moja iliyoota na pembe zingine tatu zilizoanguka mbele yake, ndiyo ile pembe iliyokuwa na macho na kinywa ambacho kilisema maneno ya kujivuna, na ambayo ilionekana kuwa kubwa kuliko pembe zingine.


Kwa maana kwa masemi yao ya kujivuna na yasiyokuwa na maana, na kwa njia ya tamaa zao mbaya za kimwili, wanawavuta watu ambao wanaanza kuwaepuka, na wale wanaoishi katika udanganyifu.


Wandugu zetu wamemushinda kwa nguvu ya damu ya Mwana-Kondoo na kwa njia ya ukweli walioshuhudia. Wao walikubali kutoa maisha yao mpaka kufa.


Kufuatana na vile ulivyojichunga katika uvumilivu sawa nilivyokuagiza, mimi vilevile nitakuchunga na hasara wakati itakapokuja katika dunia yote kwa kuwajaribu wakaaji wake.


Muache kujisifu, muache kusema kwa kiburi. Maana anayejua ni Yawe. Yeye anayapima matendo yote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ