Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 14:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Mutu mupotovu atavuna matunda ya mwenendo wake, naye mutu muzuri atapata malipo ya matendo yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 14:14
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yeye alipenda kulaani watu; laana imupate yeye mwenyewe. Hakuwatakia wengine baraka; basi, asipate baraka yeye mwenyewe.


Mutu anafanikiwa kutokana na maneno yake kama vile anavyopata matokeo ya kazi za mikono yake.


Wenye haki hawapatwi na jambo lolote baya, lakini waovu wanapata hasara nyingi.


Moyo unajua uchungu wake wenyewe, wala mugeni hawezi kushiriki furaha yake.


Mujinga anaamini kila kitu anachoambiwa, lakini mwenye akili anachunguza hatua zake zote.


Maneno ya mutu yanaweza kumushibisha; anatosheka kwa matokeo ya maneno yake.


Kama una hekima, itakufaa wewe mwenyewe; kama ukiizarau, wewe mwenyewe utapata hasara.


Yawe anasema hivi: Alaaniwe mutu anayemutegemea mwanadamu, mutu ambaye anategemea nguvu za mwanadamu, mutu ambaye moyo wake umegeuka mbali nami Yawe.


Uovu wako utakuazibu; na uasi wako utakuhukumu. Ujue na kutambua kwamba ni vibaya sana kuacha Bwana wako Yawe, Mungu wako, na kutokuwa na woga wangu ndani yako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.–


Mbona basi, watu hawa wameacha njia inayokuwa sawa na kuendelea katika upotovu wao? Wanashikamana na miungu yao ya uongo, na kukataa kunirudilia mimi!


Kwa hiyo nimewamwangia kasirani yangu na kwa moto wa hasira yangu nimewateketeza kulingana na matendo yao. –Ndivyo anavyosema Bwana wetu Yawe.


Waisraeli ni wenye kichwa kigumu kama punda. Kwa nini basi Mungu ashugulike na kuwachunga, kama kondoo katika shamba kubwa la kuwakulishia?


Nitawaangamiza wote walioniacha mimi Yawe, wote walioacha kunitafuta na kuniuliza shauri.


lakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayomupa, hatasikia kiu tena hata kidogo. Maji nitakayomupa yatakuwa ndani yake kama chemichemi inayotiririka maji ya uzima wa milele.”


Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.


Kila mutu achunguze mwenendo wake mwenyewe. Basi akiwa na sababu ya kujivuna, ajivune kufuatana na mwenendo wake mwenyewe pasipo kujilinganisha na mutu mwingine.


Anayepanda kwa kupendeza hali yake ya kimwili, atavuna matunda yanayotokana na hali ile, nayo ni lufu. Lakini anayepanda kwa kupendeza Roho Mutakatifu, atavuna matunda yanayotokana na Roho yule, nayo ni uzima wa milele.


Basi wandugu zangu, muangalie vizuri, kati yenu kusikuwe mutu mumoja mwenye moyo mubaya wa kutokuamini, aliyefikia hata kujitenga mbali na Mungu Mwenye Uzima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ