12 Kuna njia inayozaniwa kuwa sawa, lakini kwa mwisho inaongoza kwenye kifo.
Halafu Yeroboamu akaanza kufikirifikiri: “Sasa ufalme utarudi kwa jamaa ya mufalme Daudi
Basi, kisha kushauriana na wengine, akatengeneza sanamu mbili za zahabu. Kisha akawaambia watu: “Enyi watu wa Israeli, hii ndiyo miungu yenu iliyowatoa katika inchi ya Misri! Hakuna sababu ya kwenda Yerusalema kutoa sadaka kule.”
Mupumbafu anaona njia yake kuwa sawa, lakini mwenye hekima anasikiliza shauri.
Kuna njia mutu anayoona kuwa sawa, lakini kwa mwisho inaongoza kwenye kifo.
Kuna watu ambao wanajiona kuwa safi, kumbe bado hawajatakaswa uchafu wao.
“Mufanye nguvu muingie kwa kupitia mulango unaokuwa mwembamba; maana ninawaambia ninyi hakika: watu wengi watajaribu kuingia lakini hawataweza.
Basi mulipata faida gani kwa kufanya mambo yale munayopata haya juu yake sasa? Maana mwisho yao ni kifo!
Kama mutu akijizania kwamba yeye ni kitu, ijapokuwa yeye si kitu, anajidanganya yeye mwenyewe.
Mutu asiwadanganye na maneno yasiyokuwa na maana; kwa sababu ya makosa kama hayo, Mungu anawaazibu kwa kasirani yake wale wasiomutii.
Musijidanganye ninyi wenyewe kwa kusikiliza tu neno la Mungu, lakini mulitimize kwa matendo.