11 Nyumba ya mutu mwovu itabomolewa, lakini hema ya watu wa usawa itaimarishwa.
Wote wasiomwogopa Mungu hawatapata watoto, moto utateketeza mahema ya wanaokula kituliro.
Hayo ndiyo yanayowapata wasiomujali Mungu; pale ndipo pahali pa wasiomujua Mungu.
Ninyi munauliza: “Iko wapi nyumba ya yule mukubwa? Iko wapi nyumba mwovu alimoishi?”
Wanaegemea nyumba yao lakini haitasimama, wanaishikilia lakini haidumu.
Wale wanaokuchukia watapata haya, makao ya waovu yatatoweka kabisa.
kama wewe uko safi ndani ya moyo na wa usawa, kweli Mungu atakuja kukusaidia, na kukujalia makao unayostahili.
Muke wako atakuwa kama muzabibu wenye matunda mengi; watoto wako kama vichipukizi vya muzeituni kuzunguka meza yako.
Bado kidogo, mwovu atatoweka; utamutafuta pale alipokuwa, wala hautamwona.
Anayetegemea mali zake ataanguka, lakini mwenye haki atastawi kama jani bichi.
Waovu wanaangamizwa na kutoweka kabisa, lakini jamaa ya wenye haki itasimama.
Yawe anabomoa makao ya wenye kiburi, lakini analinda mipaka ya makao ya mujane.
Mwenye haki anajua yanayokuwa katika nyumba ya waovu: waovu wanaangushwa chini na kuangamia.
Katika nyumba ya mwenye hekima kuna hazina za bei kali, lakini mupumbafu anaponda mali yake yote.
Yawe analaani nyumba za waovu, lakini anabariki makao ya wenye haki.
Yawe wa majeshi anasema kwamba yeye mwenyewe ataipeleka laana hiyo. Itapenya kila nyumba ya mwizi na kila nyumba ya mwenye kuapa uongo kwa kutumia jina lake; itakaa mule na kuteketeza nyumba hiyo yote, mbao na mawe.