Alitwaa watu wote wa Yerusalemu: wakubwa wote, watu wote waliokuwa mashujaa, wafungwa elfu kumi, na wafundi wote na wafuaji wa vyuma. Hakuna aliyebaki isipokuwa wale waliokuwa wamasikini kabisa katika inchi.
Nebuzaradani, mukubwa wa walinzi wa mufalme, aliwaacha katika inchi ya Yuda watu wamoja wamasikini ambao hawakukuwa na kitu chochote, akawagawanyia mashamba ya mizabibu na kuwapa maeneo ya kulima wakati huohuo.
Lakini kulikuwa watu kumi katika kundi hilo waliomwambia Isimaeli hivi: Tafazali usituue, maana tuna akiba kubwa ya ngano, shayiri, mafuta na asali ambayo tumeificha katika pori. Basi hao akawaacha wazima.