Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 13:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Haki inalinda wenye mwenendo sawa, lakini zambi inaangusha waovu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 13:6
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Solomono akasema: “Nikimwona kuwa mwaminifu basi, hatapata hasara yoyote. Lakini nikimwona kuwa mwovu, hakika atakufa.”


Tendo hili likakuwa zambi ambayo ilisababisha ukoo wa Yeroboamu ufutiliwe mbali na kuangamizwa.


Kwa sababu alitolea sadaka kwa miungu ya Damasiki iliyokuwa imemushinda katika vita akisema: “Kwa sababu miungu ya Suria iliwasaidia wafalme wa Shamu, nikiitolea sadaka labda itanisaidia nami vilevile.” Lakini ilisababisha kuangamia kwake na taifa lote la Israeli.


Heri watu wanaoishi katika ukamilifu, wanaofuata sheria ya Yawe.


Makaa ya moto yawaangukie; watumbukizwe katika mashimo, wasiinuke tena.


Ni mutu anayefanya hivi: anaishi katika ukamilifu, anatenda kwa haki siku zote, anasema ukweli kutoka ndani ya moyo, hatetani, hatendei rafiki yake uovu, hamutukani jirani yake, anazarau wapotevu, anaheshimu wanaomwabudu Yawe, hageuzi kiapo chake hata kikimuletea hasara, hakopeshi feza yake kwa kupata faida, wala kupokea kituliro kumutesa asiyekuwa na kosa. Mutu anayefanya vile, hatatikisika hata kidogo.


Ukamilifu na usawa vinanikinga, maana ninakutumainia wewe.


Zaburi ya Daudi. Ee Yawe, unitetee, maana nimeishi katika ukamilifu, nimekutumainia wewe bila kusita.


Yawe ni kimbilio la watu wenye mwenendo sawa, lakini ataangamiza watenda maovu.


Wenye nia mbaya ni chukizo kwa Yawe, lakini wenye mwenendo mukamilifu ni furaha yake.


Ukamilifu wa watu wa usawa unawaongoza. Upotovu wa wadanganyifu unawaangamiza.


Mwenye haki anajua yanayokuwa katika nyumba ya waovu: waovu wanaangushwa chini na kuangamia.


Mutu mwovu ananaswa kwa uovu wake mwenyewe; anakamatwa na vifungo vya zambi yake mwenyewe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ