3 Anayechunga kinywa chake analinda maisha yake, mwenye midomo mirefu anajiletea maangamizi.
Ee Yawe, ulinde kinywa changu, uweke mulinzi kwenye mulango wa kinywa changu.
Unatamani kufurahia maisha, kuishi maisha marefu na kufurahia mazuri?
Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa Yedutuni. Zaburi ya Daudi.
Wenye hekima wanalinda maarifa, lakini kusemasema kwa mupumbafu kunaleta maangamizi haraka.
Kwenye kuwa maneno mengi hakukosekani makosa, lakini aneyezuia ulimi wake ana akili.
Mwenye hekima anakubali maonyo, lakini mupumbafu anayesemasema mingi ataangamia.
Mutu mwovu ananaswa kwa uongo wake mwenyewe, lakini mwenye haki anatoka katika taabu.
Muvivu anatamani lakini hapati kitu chochote, wakati mwenye bidii anajaliwa kwa wingi.
Ndani ya kinywa cha mupumbafu kunatokea maneno ya kiburi, lakini mwenye hekima analindwa na maneno yake.
Ulimi una nguvu ya kuleta uzima na kuua; wanaopenda kuutumia watakula matunda yake.
Kinywa cha mupumbafu kinamwangamiza mwenyewe; mudomo wake ni mutego wa kumunasa yeye mwenyewe.
Mupiga domo hafichi siri. Kwa hiyo umwepuke mutu wa kusemasema.
Anayechunga kinywa chake na ulimi wake, anajiepusha na matatizo.
Kama mutu akizani kwamba yeye ni mutu wa dini naye hawezi kuzuiza ulimi wake, anajidanganya mwenyewe, nayo dini yake haina faida.
Samusoni akamujibu: “Wakinifunga kwa kamba nyipya ambazo hazijatumiwa, nitakuwa zaifu kama mutu yeyote.”
hakuweza kuvumilia, akamufunulia siri yake, akisema: “Nywele zangu hazijapata kunyolewa hata kidogo. Mimi nimewekwa Munaziri wa Mungu tangu katika tumbo la mama yangu. Kama nikinyolewa nguvu zangu zitanitoka, nami nitakuwa zaifu kama mutu yeyote.”