Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 13:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Mutu muzuri anawaachia wazao wake urizi, lakini mali ya mwenye zambi imelundikiwa wenye haki.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 13:22
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo, musiwaoeshe na wabinti zenu kwa watu hao, wala musiwaruhusu wana wenu kuwaoa wabinti zao. Pia, musishugulikie usalama au mafanikio yao, kusudi ninyi wenyewe mupate kuwa na nguvu, na mufaidie mema ya inchi hiyo na kuwaachia watoto wenu kama vile urizi milele.’


Lakini wewe unabaki sawasawa, na maisha yako hayana mwisho.


Wazao wake watakuwa wenye nguvu katika inchi; watoto wa watu wa usawa watapata baraka.


Uishi na hata uwaone wajukuu wako! Amani ikuwe na Israeli!


Nilikuwa kijana na sasa mimi ni muzee; hata kidogo sijaona mutu wa haki ameachwa na Mungu, au watoto wake wakiombaomba chakula.


Taji la sifa la wazee ni wajukuu wao. Heshima ya wana ni baba yao.


Anayeongeza mali yake kwa mazidio na kulipisha faida, anamukusanyia mwingine mwenye kuwahurumia wamasikini.


Mungu anamujalia mutu anayependezwa naye hekima, akili na furaha; lakini anamupa mwenye zambi kazi ya kuvuna na kulundika, kisha Mungu anavipatia yule anayemupendeza. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ