Hao vijana wakamujibu: “Watu hao waliokuambia baba yako aliwabebesha muzigo muzito, wakakuomba uwapunguzie muzigo ule, wewe uwaambie hivi: ‘Kidole changu kidogo cha mwisho ni kinene zaidi kuliko kiuno cha baba yangu.
Kisha akamwuliza Yosafati: “Utaandamana nami kwa kupigana kule Ramoti-Gileadi?” Naye Yosafati akamujibu mufalme wa Israeli: “Ndiyo, mimi na wewe ni mutu mumoja, watu wangu ni watu wako, farasi wangu ni farasi wako.”
Lakini nabii Yehu mwana wa Hanani, akakwenda kukutana na mufalme, akamwambia: “Unazani ni vema kuwasaidia waovu na kuwapenda wanaomuchukia Yawe? Mambo uliyofanya yamekuletea kasirani ya Yawe.
Alitenda maovu mbele ya Yawe kama vile jamaa ya Ahabu ilivyofanya maana hao ndio waliokuwa washauri wake nyuma ya kifo cha baba yake, mpaka kwa kuangamia kwake.
Halafu watu wanaomutii Yawe walizungumuza wao kwa wao, naye Yawe akasikia mazungumuzo yao. Mbele yake kukawekwa kitabu ambamo uliandikwa ukumbusho wa wale wanaomutii na kumuheshimu.
Kisha nikasikia sauti ingine kutoka mbinguni ikisema: “Mutoke katika muji ule ninyi watu wangu, kusudi musishiriki zambi zake na kupatwa vilevile na mapigo yatakayoupata.