Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 13:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mutu muzuri anapata uzuri kutokana na maneno yake, lakini mudanganyifu anaishi kwa kutesa kwa ukali.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 13:2
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Makaa ya moto yawaangukie; watumbukizwe katika mashimo, wasiinuke tena.


Mungu mwenyewe ndiye mwamuzi; anamushusha mumoja na kumwinua mwingine.


Wao wanavizia na kujiangamiza wao wenyewe, wanatega mutego wa kujinasa wao wenyewe.


Basi, mutakula matunda ya mienendo yenu, mutageukiwa na mashauri yenu wenyewe.


Kinywa cha mwenye haki ni chemichemi ya uzima, lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na mateso makali.


Matazamio ya wenye haki yana matokeo mazuri; tamaa za waovu zinaleta kasirani.


Mutu anafanikiwa kutokana na maneno yake kama vile anavyopata matokeo ya kazi za mikono yake.


Maneno ya mutu yanaweza kumushibisha; anatosheka kwa matokeo ya maneno yake.


Ulimi una nguvu ya kuleta uzima na kuua; wanaopenda kuutumia watakula matunda yake.


Maana uovu ndicho chakula chao, mateso makali ndiyo divai yao.


Lakini ninyi mumepanda uovu, ninyi mumevuna ubaya; mumekula matunda ya uongo wenu. Wewe Israeli ulitegemea nguvu zako mwenyewe, na wingi wa waaskari wako.


Mateso uliyoyatenda kule Lebanoni yatakulemea wewe; uliwaua nyama, nyama nao watakuogopesha. Yote hayo yatakupata wewe, kwa mauaji na mateso uliyoitendea dunia, uliyoifanyia miji na wakaaji wake wote.


Wewe umenyanganya mataifa mengi, lakini wote wanaobaki watakunyanganya wewe, kwa mauaji na mateso uliyoitendea dunia, uliyoifanyia miji na wakaaji wake wote.


Watu hawa walimwanga damu ya watu wako na ya manabii wako, kwa sababu hiyo sasa umewakunywesha damu, nao wanastahili kutendewa vile!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ