Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.
Kwa hiyo, tufanye agano na Mungu wetu, tuachane na wanawake hawa pamoja na watoto wao, kwa kufuatana na shauri lako na la wengine wanaotii amri za Mungu. Yote yatendeke kwa kufuatana na Sheria.
Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.
Azaria mwana wa Hosaya, Yohana mwana wa Karea na watu wote wenye kiburi, walimwambia Yeremia: Yawe, Mungu wetu, hakukutuma wewe utuambie tusiende Misri, tuishi huko.
Lakini Waisraeli waliniasi kule katika jangwa; hawakuyafuata masharti yangu, lakini walikataa maagizo yangu ambayo mutu akiyafuata ataishi. Sabato zangu walizikufuru siku zote, nami nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuwaangamiza kulekule katika jangwa.
Nilifanya hivyo kwa sababu waliyakataa maagizo yangu, hawakufuata masharti yangu, wakazikufuru Sabato zangu; maana walijitoa kwa moyo juu ya sanamu za miungu yao.
Halafu watu wanaomutii Yawe walizungumuza wao kwa wao, naye Yawe akasikia mazungumuzo yao. Mbele yake kukawekwa kitabu ambamo uliandikwa ukumbusho wa wale wanaomutii na kumuheshimu.