Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 13:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Anayezarau mashauri anajiletea maangamizi, lakini anayetii amri atapewa zawadi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 13:13
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.


Kwa hiyo, tufanye agano na Mungu wetu, tuachane na wanawake hawa pamoja na watoto wao, kwa kufuatana na shauri lako na la wengine wanaotii amri za Mungu. Yote yatendeke kwa kufuatana na Sheria.


atawabariki wote wanaomwabudu, atawabariki wakubwa kama vile wadogo.


Wanaopenda sheria yako wana amani kubwa; hakuna kinachoweza kuwaangusha.


Yanatamanika kuliko zahabu, kuliko zahabu safi kabisa. Ni matamu kuliko asali, kuliko asali safi kabisa.


Yananifundisha mimi mutumishi wako; kuyafuata kunaniletea zawadi kubwa.


Wakubwa wamoja wa mufalme wa Misri wakaogopa maneno hayo ya Yawe, wakawapeleka watumwa na nyama wao ndani ya nyumba pahali pa usalama.


mumetupilia mashauri yangu yote, mumezarau maonyo yangu.


Tumaini la kungojangoja linaumiza moyo, lakini tazamio linalotimia ni musingi wa uzima.


Wanaotenda zambi wanapatwa na hasara, lakini wenye haki wanafanikiwa.


Anayefikiri sana juu ya neno atafanikiwa. Heri mutu yule anayemutumainia Yawe.


Anayeshika amri analinda maisha yake; anayezarau agizo atakufa.


Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Azaria mwana wa Hosaya, Yohana mwana wa Karea na watu wote wenye kiburi, walimwambia Yeremia: Yawe, Mungu wetu, hakukutuma wewe utuambie tusiende Misri, tuishi huko.


Lakini Waisraeli waliniasi kule katika jangwa; hawakuyafuata masharti yangu, lakini walikataa maagizo yangu ambayo mutu akiyafuata ataishi. Sabato zangu walizikufuru siku zote, nami nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuwaangamiza kulekule katika jangwa.


Nilifanya hivyo kwa sababu waliyakataa maagizo yangu, hawakufuata masharti yangu, wakazikufuru Sabato zangu; maana walijitoa kwa moyo juu ya sanamu za miungu yao.


kwa sababu hawakufuata maagizo yangu, lakini waliyakataa masharti yangu, wakazikufuru Sabato zangu na kuziabudu sanamu za miungu ya wazee wao.


Halafu watu wanaomutii Yawe walizungumuza wao kwa wao, naye Yawe akasikia mazungumuzo yao. Mbele yake kukawekwa kitabu ambamo uliandikwa ukumbusho wa wale wanaomutii na kumuheshimu.


Maana amekataa neno la Yawe na kuvunja moja kati ya amri zake. Mutu huyo atatengwa mbali kabisa; na lazima ya kifo chake itakuwa juu yake mwenyewe.


Mufurahi na kushangilia, kwa sababu munawekewa zawadi kubwa mbinguni. Ni hivi walivyowatesa manabii walioishi mbele yenu.


Lakini Abrahamu akamwambia: ‘Kama wandugu zako hawasikilizi maonyo ya Musa na ya manabii, hawatasadiki hata mutu aliyefufuka.’ ”


Basi, mujiangalie wenyewe, kusudi musipoteze matunda ya kazi yenu, lakini mupokee zawadi kamili.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ