6 Maneno ya waovu shabaha yake ni kuua, lakini kinywa cha mutu wa usawa kinaokoa.
Mawazo ya mwenye haki ni ya haki; mashauri ya mwovu ni ya udanganyifu.
Ndani ya kinywa cha mupumbafu kunatokea maneno ya kiburi, lakini mwenye hekima analindwa na maneno yake.
Muko mbio kutenda maovu, muko wepesi kumwanga damu isiyokuwa na kosa. Mawazo yenu ni mawazo ya uovu, popote munapokwenda munaacha ukiwa na uharibifu.
Hakika, kati ya watu wangu kuna waovu, watu ambao wananyanganya mali za wengine. Wako kama wawindaji wa ndege: wanatega mitego yao na kuwanasa watu.
Kesho yake kulipokucha, Wayuda wakafanya shauri; wakafanya kiapo kwamba hawatakula wala kunywa mpaka wamwue Paulo kwanza.
Basi sasa, ninyi pamoja na Baraza Kubwa mumwombe jemadari awaletee Paulo, mukimwambia tu kwamba munataka kuchunguza vizuri zaidi maneno yake. Na sisi tuko tayari kumwua mbele hajafika hapa.”
Wakamusihi Festo awafanyie wema kwa kuwaletea Paulo Yerusalema, kwa maana walikuwa wakivizia kumwua katika njia.