4 Muke mwema ni taji la utukufu kwa mume wake. Anayemupatisha mume wake haya ni kama kidonda ndani ya mifupa yake.
Mwanamuke muzuri asiyekuwa na akili ni kama pete ya zahabu kwenye pua la nguruwe.
Mawazo ya mwenye haki ni ya haki; mashauri ya mwovu ni ya udanganyifu.
Mwanamuke mwenye hekima anajenga nyumba yake, lakini mupumbafu anaibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
Amani ndani ya roho inamupa mutu afya, lakini wivu inaozesha mifupa.
Anayemupata muke amepata kizuri; ni zawadi kutoka kwa Yawe.
Afazali kuishi katika jangwa kuliko kukaa na mwanamuke mugomvi na muchokozi.
Afazali kuishi pembeni juu ya paa, kuliko kuishi ndani ya nyumba pamoja na mwanamuke mugomvi.
mwanamuke asiyependwa anayeolewa; na mujakazi anapotwaa nafasi ya bibi yake.
Anasema: “Wanawake wengi wametenda mambo ya ajabu, lakini wewe umewashinda wote.”
Nikasikia hayo, matumbotumbo yangu yakatetemeka. Midomo yangu inatetemeka kwa hofu, mifupa yangu inateguka, miguu yangu inatetemeka. Ninangojea kwa utulivu siku ile ya hasara, ambayo inawafikia wale wanaotushambulia.
Lakini katika ushirika wetu na Bwana, hakuwezi kuwa mwanamuke pasipo mwanaume wala mwanaume pasipo mwanamuke.
Mwanaume hapaswi kufunika kichwa, kwa sababu yeye ni mufano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamuke ni utukufu wa mwanaume.
Sasa binti yangu usifazaike, nitakufanyia lolote utakaloomba kwa sababu kila mutu katika muji huu anajua wema wako.