Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 12:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Anayependa mafundisho anapenda maarifa, lakini asiyependa kuonywa ni mujinga.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 12:1
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Unifundishe namna ya kushika kanuni zako, nami nitafikiri juu ya matendo yako ya ajabu.


Afazali mutu mwema anipige kwa kunionya; lakini sikubali hata kidogo kusifiwa na wabaya, maana ninaomba siku zote juu ya maovu yao.


Usikuwe mupumbafu kama farasi au nyumbu, ambao lazima wafungwe kamba ndani ya kinywa, kama sivyo hawatakukaribia.”


Wewe unachukia maonyo, na maneno yangu haupendi kuyafuata.


Matendo yako, ee Yawe, ni makubwa sana! Mawazo yako hayatambulikani!


Mwenye hekima anakubali maonyo, lakini mupumbafu anayesemasema mingi ataangamia.


Ikiwa mwenye haki anapata malipo hapa katika dunia, hakika mwovu na mwenye zambi watalipwa!


Mutu muzuri anapata rehema za Yawe, lakini mwenye nia mbaya analaaniwa na Mungu.


Azabu kali ni kwa wanaoacha mwenendo mwema; yeyote anayechukia kuonywa atakufa.


Anayejitenga na wenzake anajipendelea mwenyewe; anakasirika akipewa shauri lolote jema.


Mimi ni mupumbafu sana, wala si mutu; sina akili ya mwanadamu.


Ninawapenda wale wanaonipenda; wanaonitafuta kwa bidii wananipata.


“Sasa basi, wana wangu, munisikilize: heri wale wanaofuata njia zangu.


Asiyenipata anajizuru mwenyewe; wote wanaonichukia wanapenda kifo.”


Ngombe anamufahamu mwenye naye, punda anajua kibanda cha bwana wake; lakini Waisraeli hawajui, watu wangu, hawaelewi!


Kuhani atamwangalia na kama kivimba cheupe ambacho kimefanya nywele zake zikuwe nyeupe na kivimba kile kimegeuka kuwa kidonda kibichi,


Atatumia ubaya wa kila namna kwa kuwadanganya wale wanaopotea kwa sababu hawakupenda kukubali na kupenda mambo ya kweli yaliyoweza kuwaokoa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ