7 Mwovu akikufa, tumaini lake nalo linatoweka. Tumaini la asiyemwogopa Mungu ni la bure.
Lakini waovu macho yao yatafifia, njia zote za kutorokea zitawapotea; tumaini lao la mwisho ni kukata roho!
Watu waovu wanaona hayo na kuuzika. Wanasaga meno kwa chuki na kutoweka. Matumaini ya mutu mubaya yanapotea bure.
Mwanadamu akitoa pumzi yake ya mwisho, anarudi katika mavumbi alimotoka, na hapo mipango yake yote inatoweka.
Tumaini la mwenye haki linaleta furaha, lakini tazamio la mwovu linapotea bure.
Yawe ni kimbilio la watu wenye mwenendo sawa, lakini ataangamiza watenda maovu.
Mutu wa haki anaokolewa katika shida, na mwovu anaingia mule kwa pahali pake.
Mwovu anaangamizwa kwa matendo yake maovu, lakini mwenye haki atapata usalama kwa uaminifu wake.
Utaendelea kujiona kuwa mungu mbele ya hao watakaokuua? Katika mikono ya hao watakaokuangamiza, utatambua kwamba wewe ni mutu tu, wala si mungu!