30 Tunda la mwenye haki ni muti wa uzima, na mwenye hekima anavuta watu.
Kama miti iliyopandwa katika nyumba ya Yawe, wanastawi katika viwanja vya Mungu wetu;
Matumaini ya waovu yanaporomoka na kuharibika, lakini mutu mwenye haki anasimama imara.
Mushuhuda wa kweli anaokoa maisha, lakini musema uongo ni mudanganyifu.
Ulimi mupole ni musingi wa uzima, lakini uovu wake unavunja moyo.
Hekima ni muti wa uzima kwa wote wanaoipata; wana heri wote wanaoshikamana nayo.
Wale wenye hekima watangaa kama vile anga linavyongaa, na wale waliowaongoza wengine kutenda mema, watangaa kama nyota milele.
Yesu akawaambia: “Munifuate, nami nitawaweka kwa kazi ya kuopoa watu.”
Muvunaji anakwisha kupokea mushahara, naye anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele, kusudi mupandaji na muvunaji wafurahi pamoja.
Ninyi peke yenu tu ndio tumaini, furaha, na taji ya ushindi tutakavyojivunia wakati Bwana Yesu Kristo atakaporudia.
mukumbuke neno hili: yule anayemurudisha mwenye zambi toka njia ya upotevu ataokoa roho ya yule kutoka kifo, na zambi nyingi zitasamehewa.
“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda nitamupa ruhusa ya kula matunda ya muti wa uzima unaokuwa katika bustani ya Mungu!