26 Watu wanamulaani mutu anayeficha ngano, lakini wanamutakia baraka mwenye kuiuzisha.
Wakati ule Yosefu alikuwa mukubwa kule Misri. Yeye ndiye aliyekuwa akiwauzishia wanainchi ngano. Basi, kaka zake wakakuja na kuinama mbele ya Yosefu kwa heshima.
Yosefu akakusanya feza yote ya inchi ya Misri na Kanana kutokana na ngano waliyonunua, akapeleka feza hiyo kwa nyumba ya mufalme.
Waliokuwa karibu kuangamia walinitakia baraka. Niliwafanya wajane waone tena furaha ndani ya moyo.
Mwenye haki anajiletea baraka yeye mwenyewe, lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na mateso makali.
Anayemwachilia mutu mwenye kosa analaaniwa na watu na kuchukiwa na mataifa.
Anayesaidia wamasikini hatakosewa kitu, lakini anayekataa kuwaangalia atalaaniwa kwa wingi.