25 Mutu anayetoa kwa moyo safi atafanikishwa. Mutu anayekunywesha mwingine maji, naye atakunyweshwa.
Kuna watu wanaotoa mali yao kwa wingi na kuzidi; lakini wachoyo wanazilinda na kuendelea katika umasikini.
Muchoyo anachochea magomvi, lakini anayetegemea Yawe atafanikiwa.
Anayesaidia wamasikini hatakosewa kitu, lakini anayekataa kuwaangalia atalaaniwa kwa wingi.
Kwa hiyo gala zako zitajaa ngano, na mitungi yako itafurika na divai mupya.
Umuheshimu Yawe kwa mali yako, na kwa malimbuko ya mazao yako yote.
Lakini wenye heshima wanatenda mambo ya heshima, nao wanatetea mambo yenye heshima.
Heri wale wanaokuwa na huruma, maana Mungu atawahurumia!