Azaria, Kuhani Mukubwa aliyekuwa wa uzao wa Sadoki akamujibu: “Tangu wakati watu walipoanza kuleta matoleo yao katika hekalu, tumekuwa na vyakula vya kutosha na hata tuna akiba kubwa. Yawe amewabariki watu wake, ndiyo maana tumepata vitu hivi vyote.”
Munapanda mbegu kwa wingi, lakini munavuna kidogo. Munakula, lakini hamushibi. Munakunywa divai, lakini hamutosheki. Munavaa nguo, lakini bado munasikia baridi. Mushahara wa mutumishi unakuwa kama umetumbukizwa katika mufuko uliotoboka.
Ninawajibia hivi: Ni sawa kwa mutu kumudanganya Mungu? Hapana! Lakini ninyi munanidanganya! Ingawa hivyo ninyi munauliza: Tunakudanganya kwa namna gani? Kweli! Munanidanganya juu ya zaka na sadaka zenu.
Mumupe ndugu masikini kwa moyo safi bila kunungunika, maana kwa ajili ya hayo, Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika kazi zenu zote na katika kila munalofanya.