23 Matazamio ya wenye haki yana matokeo mazuri; tamaa za waovu zinaleta kasirani.
Ee Yawe, unapokea maombi ya muzaifu; unamutia moyo na kumutegea sikio.
Ninakutafuta kwa moyo wote; usiniachilie kugeuka mbali na amri zako.
Heri mwenendo wangu ungeimarika kwa kuyafuata masharti yako!
Jambo moja nimemwomba Yawe, ninatafuta hili tu: nikae ndani ya nyumba ya Yawe siku zote za maisha yangu, niuone uzuri wa Yawe, na kutafuta maongozi yake ndani ya hekalu lake.
Uitafute furaha yako kwa Yawe, naye atakujalia unayotamani katika moyo.
Tumaini la mwenye haki linaleta furaha, lakini tazamio la mwovu linapotea bure.
Kuna watu wanaotoa mali yao kwa wingi na kuzidi; lakini wachoyo wanazilinda na kuendelea katika umasikini.
Mwovu akikufa, tumaini lake nalo linatoweka. Tumaini la asiyemwogopa Mungu ni la bure.
Mawazo ya mwenye haki ni ya haki; mashauri ya mwovu ni ya udanganyifu.
Mutu muzuri anapata uzuri kutokana na maneno yake, lakini mudanganyifu anaishi kwa kutesa kwa ukali.
Moyo wangu unakutamani usiku kucha, nafsi yangu inakutafuta kwa moyo. Utakapohukumu dunia, watu wote katika ulimwengu watajifunza haki.
Sikukukaza kutenda mabaya, wala sikutamani ile siku ya hasara ifike. Wewe mwenyewe unajua maneno niliyosema mbele yako.
Heri wale wanaokuwa na njaa na kiu ya kufanya yanayokuwa haki, maana watashibishwa!
Lakini inayobaki tu ni kungojea kwa woga hukumu na moto mukali wa Mungu utakaowateketeza waasi.