20 Wenye nia mbaya ni chukizo kwa Yawe, lakini wenye mwenendo mukamilifu ni furaha yake.
Ninajua, Mungu wangu, kwamba wewe unapima moyo, nawe unapendezwa na uaminifu. Nami, katika uaminifu wa moyo wangu nimetoa vitu hivi vyote kwa mapenzi yangu, na sasa ninaona watu wako wanaokuwa hapa, wakikutolea kwa mapenzi yao na furaha.
Upotovu wowote ukuwe mbali nami; sitahusika kabisa na uovu.
Yawe ni wa haki na anapenda watu watende kwa haki. Watu wa usawa wataona uso wake.
Heri watu wanaoishi katika ukamilifu, wanaofuata sheria ya Yawe.
Ninajua kwamba Yawe anatetea wamasikini na kuwapatia wakosefu haki.
Nimekukosea wewe peke yako, nimetenda mabaya mbele yako. Hivi uamuzi wako ni wa haki, hukumu yako haipotoki.
Hakika mwovu hataepuka kuazibiwa, lakini wenye haki wataokolewa.
Kinywa kinachosema uongo ni chukizo kwa Yawe, lakini watu waaminifu ni furaha yake.
Haki inalinda wenye mwenendo sawa, lakini zambi inaangusha waovu.
Wapumbafu wanafurahia zambi, lakini watu wa usawa wanapata rehema kwa Mungu.
Mawazo ya mwovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maneno mema yanamufurahisha.
Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.
Njia ya watu wa usawa ni kujiepusha na uovu; anayechunga njia yake anachunga maisha yake.
Mutu mwovu anajionyesha kuwa hodari, lakini mutu wa usawa anafikiri vizuri juu ya mwenendo wake.
Maana waovu ni chukizo kwa Yawe, yeye anawafanya watu wa usawa kuwa warafiki zake.
Akiwa amejaa mabaya ndani ya moyo, anatunga maovu. Anaamusha ugomvi kila pahali.
Kumwogopa Yawe ni kuchukia uovu. Ninachukia kiburi, majivuno maisha mabaya, na luga mbaya.
Anayemwonya mwenye kiburi anapata mazarau, anayekaripia mwovu anajiletea matusi.