Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 11:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Mutu anayekusudia kuwa mwenye haki ataishi, lakini anayechagua kutenda maovu atakufa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 11:19
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Akamwambia mufalme: “Yawe anasema hivi: ‘Kwa sababu ulituma wajumbe kuomba shauri kwa Bali-Zabubu mungu wa Ekuroni sawa vile hakuna Mungu katika Israeli ambaye ungemwomba shauri, basi, hautashuka katika kitanda ambacho umepanda juu yake. Hakika utakufa.’ ”


Mumwambie mufalme kwamba Yawe amesema hivi: ‘Hautashuka katika kitanda ulichopanda juu yake. Hakika utakufa.’ ”


Mushahara wa mutu wa haki ni uzima, lakini mapato ya mwovu ni katika zambi.


Utajiri haufai kitu siku ya kasirani, lakini haki inaokoa kutoka kifo.


Haki ni njia ya uzima, lakini uovu unaongoza katika kifo.


Kumwogopa Yawe kunaongoza kwenye uzima; anayemwogopa anajaliwa pumziko la kutoshelea, wala hatapatwa na ubaya wowote.


Anayetangatanga mbali na njia ya ufahamu, atajikuta ametua kati ya wafu.


Anayetafuta haki na wema atapata uzima, haki, na heshima.


Asiyenipata anajizuru mwenyewe; wote wanaonichukia wanapenda kifo.”


lakini katika kila taifa mutu yeyote anayemutii Mungu na kutenda yanayokuwa ya haki, anamupendeza.


Kwa maana mushahara wa zambi ni kifo, lakini zawadi Mungu anayotoa ni uzima wa milele kwa kuungana na Yesu Kristo, Bwana wetu.


Mutafuata yanayokuwa ya haki tu, kusudi mupate kuishi na kurizi inchi munayopewa na Yawe, Mungu wenu.


Halafu ile tamaa mbaya ikisha kukomaa, inazaa zambi, nayo zambi ikisha kukomaa inazaa lufu.


Hii ndiyo njia inayoonyesha wazi tofauti kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Shetani. Mutu asiyetenda mambo ya haki au asiyemupenda ndugu yake si mutoto wa Mungu.


Watoto wangu, mutu asiwadanganye! Mutu anayetenda mambo ya haki ni mwenye haki kama vile Kristo ni mwenye haki.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ