14 Pasipo uongozi taifa linaanguka; kwenye kuwa washauri wengi kuna usalama.
Basi, kama ukitaka kuyaokoa maisha yako na ya mwana wako Solomono, ninakushauria hivi:
Alitenda maovu mbele ya Yawe kama vile jamaa ya Ahabu ilivyofanya maana hao ndio waliokuwa washauri wake nyuma ya kifo cha baba yake, mpaka kwa kuangamia kwake.
Mipango inaharibika kwa kukosa shauri, lakini kwa washauri wengi, inasimama.
Hekima ni chemichemi ya uzima kwa yule anayekuwa nayo, lakini upumbafu ni azabu ya wapumbafu.
Mipango mizuri inafanyika kwa kushauriana; ukitaka kuanza vita inafaa kufikiri kwanza.
Maana kwa mipango mizuri unaweza kupigana vita, na kwa washauri wengi ushindi unapatikana.