8 Mwenye hekima anakubali maonyo, lakini mupumbafu anayesemasema mingi ataangamia.
Unieleweshe nipate kushika sheria yako, niifuate kwa moyo wangu wote.
Mwenye hekima akizisikiliza, zitamwongezea elimu; na mwenye ufahamu zitamupatia ujuzi.
Anayekonyeza macho kwa nia mbaya analeta taabu, lakini anayeonya waziwazi analeta amani.
Wenye hekima wanalinda maarifa, lakini kusemasema kwa mupumbafu kunaleta maangamizi haraka.
Anayependa mafundisho anapenda maarifa, lakini asiyependa kuonywa ni mujinga.
Mutu mwovu ananaswa kwa uongo wake mwenyewe, lakini mwenye haki anatoka katika taabu.
Anayechunga kinywa chake analinda maisha yake, mwenye midomo mirefu anajiletea maangamizi.
Bidii katika kila kazi inaleta faida, lakini maneno matupu yanaleta umasikini.
Hekima ya mwenye akili inamwonyesha njia yake, lakini upumbafu wa wapumbafu unawadanganya wenyewe.
Usimwonye mwenye kiburi maana atakuchukia; umwonye mwenye hekima naye atakupenda.
Umufundishe mwenye hekima naye atazidi kuwa na hekima; umufundishe mutu wa haki naye atazidi kuwa na elimu.
Maneno ya mwenye hekima yanamupa upendeleo; lakini maneno ya mupumbafu yanamwangamiza.
Nani anayekuwa na hekima na ufahamu kati yenu? Basi aonyeshe jambo lile kwa njia ya mwenendo wake muzuri, kwa njia ya matendo yanayofanyika katika upole unaotokana na hekima ile.