31 Kinywa cha mwenye haki kinatoa mambo ya hekima, lakini ulimi wa mutu mubaya utakatwa mbali.
Ee Yawe, ukomeshe midomo hiyo ya kudanganya, na ndimi hizo zinazojigamba.
Usiniache nifezeheke, ee Yawe, maana mimi ninakulilia; lakini uwaache waovu wafezeheke, uwaache wapotelee huko kuzimu.
Mutu wa haki anasema maneno ya hekima, kwa ulimi wake anasema kufuatana na sheria ya Mungu.
Watauawa kwa upanga, maiti zao zikuwe chakula cha mbweha.
Kinywa cha mwenye haki ni chemichemi ya uzima, lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na mateso makali.
Katika kinywa cha mwenye ufahamu kuna hekima, lakini wasiokuwa na akili watapigwa fimbo katika mugongo.
Mwenye moyo mupotovu hafanikiwi, na musema uongo anapatwa na hasara.
Anafungua kinywa kwa kusema kwa hekima; anawashauri wengine kwa wema.